Pages

Ads 468x60px

Saturday, June 27, 2015

Maamuzi ya Mahakama Kuu Dar kuhusu ishu ya Chenge na ESCROW >>



Ishu ya ESCROW ni kama kuna watu wengi walianza kuisahau hivi. Jana  imerudi  tena   kwenye masikio ya watu ambapo tunakumbuka kuna orodha ya Mawaziri na Wenyeviti wa Kamati za Bunge walisimamishwa baada ya kutajwa kuhusika na mgao wa Bil. 300 zilizokuwa kwenye account ya ESCROW.
 
Mbunge Andrew Chenge alikuwa mmoja ya waliotajwa kuhusika pia, ishu ikapelekwa Kamati ya Maadili na baadae Mbunge huyo akapeleka ombi Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam ili kuzuia kuhojiwa na Kamati hiyo.
 
Jana June 26 2015 ripoti kutoka Mahakamani inasema Mahakama hiyo imetupilia mbali Ombi hilo kwa kuwa imeona haikuwa na Mamlaka ya kuzuia Shauri hilo, na walichokiona ni kwamba Chenge alikuwa na njia mbadala kushughulika na ishu hiyo badala ya kukimbilia Mahakamani.

0 comments:

Post a Comment

SHARE