Pages

Ads 468x60px

Wednesday, June 14, 2017

AUAWA KISHA KUCHOMWA MOTO KWA KUIBA KUKU MMOJA HUKO BUNDA


MWANAMUME mmoja ameuawa na mwili wake kuchomwa moto na wananchi wenye hasira katika wilaya ya Bunda mkoani Mara, kwa tuhuma ya kuiba kuku mmoja.
Kwa mujibu wa polisi wilayani Bunda, tukio hilo limetokea juzi majira ya asubuhi mjini Bunda. Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama katika wilaya ya Bunda, ambaye pia ni mkuu wa wilaya hiyo, Lydia Bupilipili, jana amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.
Alisema mwanamume huyo aliuawa na wananchi wanaojiita wenye hasira, baada ya kumkamata akiwa ameiba kuku mmoja, mali ya mkazi wa mjini hapa. Amemtaja aliyeuawa kwa kipigo na wananchi hao na kisha mwili wake kuchomwa moto kuwa ni Mwita Machanchu (30) mkazi wa Mtaa wa Mapinduzi mjini Bunda.
Hata hivyo, akizungumza baada ya kuzindua Bodi ya afya ya halmashauri ya wilaya ya Bunda, mkuu huyo wa wilaya alikemea vitendo vya mauaji vinavyotokea mara kwa mara wilayani Bunda.
Alisema kitendo cha watu kujichukulia sheria mkononi na kuondoa uhai wa watu wengine, kamwe hakivumiliki na akawataka wananchi pindi wanapowakamata wahalifu wawafikishe polisi, ili wafikishwe hatua za kisheria zichukue mkondo wake.
Aidha, amewataka wananchi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa jeshi la polisi na kwenye kamati ya ulinzi na usalama, kwa kuwataja watu wanaojihusisha na vitendo vya uhalifu ili waweze kukamatwa na kufikishwa mahakamani.

0 comments:

Post a Comment

SHARE