MTANDAO
 wa wanafunzi Tanzania (TSNP) umeipa siku saba Tume ya Taifa ya Uchaguzi
 (NEC) kutoa ufumbuzi juu ya namna gani wanafunzi wenye sifa za kupiga 
kura watakavyoandikishwa kwenye mfumo mpya wa Biometric Voters 
Registration (BVR) kufuatia kuingiliana na ratiba za masomo.
Tamko
 hilo limetolewa jana Jijini Dar es salaam, kupitia kwa Kaimu Mwenyekiti
 wa umoja huo Shitindi Venance, ambapo alisema kuwa wanaiomba tume hiyo 
ya uchaguzi  ndani ya siku saba kueleza ni kwa namna gani wanafunzi 
waliko vyuoni pamoja na wale waliko bonding wenye sifa za kupiga kura 
namna watakavyoandikishwa kutokana na ratiba za uandikishaji kupishana 
na zile za vyuo pamoja na shule za Sekondali.
Alisema
 kuwa kumekuwepo na changamoto kubwa kwa upande wa wanafunzi nchini 
zinazopelekea mtandao huo kuwa na sintofahamu juu ya hatma ya 
undikishwaji wa wanafunzi wenye sifa za kuandikishwa kwa mujibu wa 
katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania na  Nec.
“Mtandao
 huu umekuwa ukifuatilia kwa ukaribu sana mchakato wa uandikishwaji 
tangua kuanza kwake kupitia matawi yake yaliyoko mikoani matharani 
Njombe, Ruvuma, Mtwara na Mbeya na kubaini kuwa kundi la wanafunzi 
limekuwa na changamoto kubwa kwenye zoezi la uandikishwaji,
“Hii
 ni kutokana na ukweli kwamba zoezi la uandikishwaji linaendelea wakati 
huo huo wanafunzi wakiendelea na ratiba zao za masomo huku wengine 
wakiwa shule za bweni,
“Hivyo
 kama tume tunasikitika kwani tume ya uchaguzi inayatambua haya lakini 
bado haitaki kutoa mwongozo ili kuhakikisha kuwa wanafunzi wenye sifa 
wanapata haki yao ya kuandikishwa, hivyo tunatoa siku saba kuanzia kesho
 (leo) tume itupe majibu, ” alisema Venance.
Aliongeza
 kuwa ni bora NEC ikapeleka mashine (BVR)kwenye kila taasisi ya elimu 
kwaajili ya uandikishwaji wa wanafunzi wakiwa katika taasisi zao kama 
walivyofanya NIDA.
Lakini
 pia wanaiomba tume kuhakikisha kuwa inatoa majibu juu ya changamoto 
hiyo inayowakabili wanafunzi katika kwenye zoezi hilo kwani ni hatari 
kwa Amani ya Nchi endapo wanafunzi na wanavyuo watakosa haki yao ya 
kuandikishwa na hatimaye  kukosa haki yao ya kupiga kura katika uchaguzi
 ujao.
Kwa
 upande mwingine umoja huo umeitaka serikali kuanza kushughulikia vyanzo
 vya mogogoro na siyo matokeo ya migogoro hivyo watawala wa vyuo vikuu 
nchini watumie busara ya kuwarudisha wanafunzi wote waliofukuzwa na 
wengine kusimamishwa kwani ni hatari kwa amani ya nchi .

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment