Pages

Ads 468x60px

Saturday, May 30, 2015

Wanafunzi waipa Siku saba Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)



MTANDAO wa wanafunzi Tanzania (TSNP) umeipa siku saba Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kutoa ufumbuzi juu ya namna gani wanafunzi wenye sifa za kupiga kura watakavyoandikishwa kwenye mfumo mpya wa Biometric Voters Registration (BVR) kufuatia kuingiliana na ratiba za masomo.
 
Tamko hilo limetolewa jana Jijini Dar es salaam, kupitia kwa Kaimu Mwenyekiti wa umoja huo Shitindi Venance, ambapo alisema kuwa wanaiomba tume hiyo ya uchaguzi  ndani ya siku saba kueleza ni kwa namna gani wanafunzi waliko vyuoni pamoja na wale waliko bonding wenye sifa za kupiga kura namna watakavyoandikishwa kutokana na ratiba za uandikishaji kupishana na zile za vyuo pamoja na shule za Sekondali.
 
Alisema kuwa kumekuwepo na changamoto kubwa kwa upande wa wanafunzi nchini zinazopelekea mtandao huo kuwa na sintofahamu juu ya hatma ya undikishwaji wa wanafunzi wenye sifa za kuandikishwa kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania na  Nec.
 
“Mtandao huu umekuwa ukifuatilia kwa ukaribu sana mchakato wa uandikishwaji tangua kuanza kwake kupitia matawi yake yaliyoko mikoani matharani Njombe, Ruvuma, Mtwara na Mbeya na kubaini kuwa kundi la wanafunzi limekuwa na changamoto kubwa kwenye zoezi la uandikishwaji,
 
“Hii ni kutokana na ukweli kwamba zoezi la uandikishwaji linaendelea wakati huo huo wanafunzi wakiendelea na ratiba zao za masomo huku wengine wakiwa shule za bweni,
 
“Hivyo kama tume tunasikitika kwani tume ya uchaguzi inayatambua haya lakini bado haitaki kutoa mwongozo ili kuhakikisha kuwa wanafunzi wenye sifa wanapata haki yao ya kuandikishwa, hivyo tunatoa siku saba kuanzia kesho (leo) tume itupe majibu, ” alisema Venance.
 
Aliongeza kuwa ni bora NEC ikapeleka mashine (BVR)kwenye kila taasisi ya elimu kwaajili ya uandikishwaji wa wanafunzi wakiwa katika taasisi zao kama walivyofanya NIDA.
 
Lakini pia wanaiomba tume kuhakikisha kuwa inatoa majibu juu ya changamoto hiyo inayowakabili wanafunzi katika kwenye zoezi hilo kwani ni hatari kwa Amani ya Nchi endapo wanafunzi na wanavyuo watakosa haki yao ya kuandikishwa na hatimaye  kukosa haki yao ya kupiga kura katika uchaguzi ujao.
 
Kwa upande mwingine umoja huo umeitaka serikali kuanza kushughulikia vyanzo vya mogogoro na siyo matokeo ya migogoro hivyo watawala wa vyuo vikuu nchini watumie busara ya kuwarudisha wanafunzi wote waliofukuzwa na wengine kusimamishwa kwani ni hatari kwa amani ya nchi .

0 comments:

Post a Comment

SHARE