Pages

Ads 468x60px

Monday, June 1, 2015

CHADEMA Wamteua Godbless Lema kuwa Kamanda wa Operesheni ya Uandikishaji wa Daftari la Wapigakura



CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Kanda ya Kaskazini, kimemchagua Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho Godbless Lema, kama Kamanda wa Operesheni ya Uandikishaji wa Daftari la Wapigakura katika kanda hiyo.
 
Hayo yalisemwa juzi jijini hapa na Katibu wa Chadema Mkoa wa Arusha, Calist Lazaro, alipokuwa akizungumza  katika kikao maalumu cha mkakati  kilichowashirikisha viongozi wa Wilaya ya Arusha, wenyeviti wa kata na viongozi wa Chadema wa Serikali za Mitaa kutoka kata 25 za Jiji la Arusha.

“Tuweke akili zetu kwenye BVR kwani hakuna ushindi bila watu kujiandikisha, naomba nimtambulishe Lema kama Kamanda wa Operesheni ya BVR katika Kanda ya Kaskazini, ambaye ataongoza kampeni hiyo ya kuhamasisha wananchi wajiandikishe kwa wingi ili tuweze kushinda,”alisema Lazaro
 
Alisema kutokana na uhamasishaji wa Lema ambaye pia ni Mbunge wa Arusha Mjini, utakiswezesha chama hicho kushinda katika uchaguzi mkuu na hata kuongeza idadi ya majimbi kutoka mawili ya sasa.
 
Awali Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Arusha, Derick Magoma, alisema lengo la kikao hicho ni mkakati ya kuhimiza wananchi kujiandikisha kwenye daftari hilo ili kushinda katika uchaguzi huo kwa kishindo.
 
“Tusipojiandaa sasamhatutaweza kushinda uchaguzi huu,kwani tumedhamiria kushinda kwa kishindo, ndiyo maana tumeitana hapa kupanga mikakati ya ushindi ikiwa ni pamoja na kuhamasisha wananchi kujiandikisha, mwaka huu hata walete magari yenye maji ya kuwasha, mabomu, lakini ushindi ni lazima,”alisema

0 comments:

Post a Comment

SHARE