WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda, amewataka Watanzania wajiandikishe kwa wingi katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
Amesema
 kwamba, kama watafanikiwa kufanya hivyo, watakuwa na sifa za kuwachagua
 wagombea wakati wa uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 25, mwaka
 huu.
Waziri
 Mkuu Pinda aliyasema hayo juzi alipokuwa akizungumza baada ya 
kujiandikisha kwenye ofisi ya Ofisa Mtendaji wa Kata iliyopo Kijiji cha 
Kibaoni, wilayani Mpanda, Mkoa wa Katavi.
“Ninawasihi
 Watanzania wote tusiache kutumia fursa hii, kila mtu ahakikishe 
anajiandikisha kwa sababu ni fursa pekee itakayohakikisha kila mwananchi
 anashiriki uchaguzi wa kumpata rais, mbunge na diwani katika eneo lake.
“Binafsi
 nimefarijika kwa kazi inayoendelea hasa hasa katika Halmashauri za 
Nsimbo na Mlele ambazo zimefanikiwa kuandikisha watu kwa zaidi ya 
asilimia 100,” alisema Waziri Mkuu Pinda.
Awali
 akiwasilisha taarifa ya uandikishaji katika Halmashauri ya Mlele, 
Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Godwin Benne, alisema walilenga 
kuandikisha watu 19,482 lakini hadi kufikia jana walifanikiwa 
kuandikisha watu 20,292 sawa na asilimia 105.
“Kata
 ya Kibaoni ambayo ina vituo sita, jana peke yake tuliandikisha watu 
1,007 kikiwamo kituo cha Kibaoni ambacho Waziri Mkuu Pinda 
amejiandikisha,” alisema.
Alivitaja
 vituo vingine, kuwa ni Milumba, Sungusungu, Ilalangulu, Manga na Shule 
ya Msingi Kakuni ambako Mama Tunu Pinda alijiandikisha juzi hiyo hiyo.
Naye,
 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, Neneka Rashid, alisema 
uandikidhaji ulianza Mei 18, mwaka huu kwenye kata 12.
Alisema
 kwamba hadi kufikia juzi, kata nne zilikuwa zimeandikisha watu 12,001 
ambazo ni sawa na asilimia 108.9 ingawa matarajio yao yalikuwa ni 
kuandikisha watu 11,014.

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment