Pages

Ads 468x60px

Wednesday, May 27, 2015

Polisi wakamatwa kwa upotevu wa bunduki



JESHI la Polisi Mkoa wa Rukwa, linawashikilia askari polisi wawili kwa tuhuma za kuiba  bunduki aina ya SMG mali ya jeshi hilo.

Akizungumza mjini hapa jana, Kaimu Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Rukwa, Leons Rwegasira,  alisema bunduki hiyo iliibwa Mei 19 mwaka huu katika Kituo cha Polisi mjini Namanyere, Wilaya ya Nkasi.

Pamoja na kuthibitisha wizi huo, Kamanda Rwegasira hakutaka kutaja majina ya watuhumiwa kwa kile alichosema kuwa uchunguzi bado unaendelea.

“Kuna polisi wawili tunawashikilia kwa tuhuma za wizi wa bunduki na upotevu huo uligunduliwa Mei 19 mwaka huu baada ya ukaguzi wa kawaida kituoni hapo kufanyika.

“Baada ya upotevu wa silaha hiyo kuwapo, msako mkali ulianza mara moja na hatimaye silaha hiyo ilipatikana ikiwa imefukiwa chini ya ardhi.

“Kwa hiyo, watuhumiwa bado tunaendelea kuwashikilia huku upelelezi ukiendelea na utakapokamilika, tunaweza kuwafikisha mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake,” alisema Kamanda Rwegasira.

0 comments:

Post a Comment

SHARE