Rais
 Kikwete amewaongoza watanzania katika maadhimisho ya siku ya kupinga 
matumizi ya dawa za kulevya duniani yaliyofanyika kitaifa mjini Bagamoyo
 katika viwanja vya shule ya msingi Mwanamakuka.
Shughuli
 hizo zilianza kwa maandamano katika viwanja hivyo ambapo badaye mkuu wa
 mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo alimkaribisha Rais pamoja na 
wananchi waliohudhuria katika viwanja hivyo.
Katika
 hotuba yake, Rais Jakaya kikwete alisema vita dhidi ya madawa ya 
kulevya ni kubwa na inahusisha wafanyabiashara wakubwa ambapo fedha 
zinazopatikana hutumika kufadhili uhalifu wa kimataifa ikiwemo ugaidi.
Rais
 Kikwete alisema anajivunia kutungwa kwa sheria mpya ya kudhibiti na 
kupambana na dawa za kulevya ya mwaka 2015 katika serikali ya awamu ya 
nne, ambayo inaweka masharti ya kuundwa kwa chombo maalum 
kitakachoshughulikia kwa ukaribu tatizo hilo, na kwamba anataka chombo 
hicho kiwe kimeundwa kabla ya Oktoba ili kutoa baraka zake kabla 
hajaondoka madarakani, na atamkabidhi Rais ajaye aendelee kuanzia hapo.
Awali
 Waziri wa Afya na ustawi wa jamii, Dkt Seif Rashid alipata fursa ya 
kufafanua mikakati ya serikali katika kupambana na tatizo la matumizi ya
 madawa ya kulevya na kuwapiga vita wafanyabiashara wanaojihusisha na 
dawa hizo.
Naye
 Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi isiyokuwa ya serikali inayojishughulisha
 na masuala ya vijana Tanzania Youth Aliance TAYOA, Peter Masika alisema
 kwamba wamezindua namba ya simu itakayotumika kuwaelimisha vijana dhidi
 ya athari ya matumizi ya madawa ya kulevya.
Wakati
 huo huo mwanaharakati anayepambana na matumizi ya madawa ya kulevya 
Rehema Chalamila – Ray C aliwataka vijana wenzake waliojitumbukiza 
katika janga hili waweze kufuata mfano wake na wajitokeze kutokomeza 
janga hili kwa kutumia dawa za Methadoni na kuacha kabisa madawa.
Katika
 maadhimisho hayo ambayo yaliyoongozwa na kauli mbiu ya tujenge jamii na
 maisha ya utu bila dawa za kulevya, Rais kikwete alihimiza ushirikiano 
kwa jamii katika kupinga matumizi ya dawa za kulevya kwa vijana na 
kutokomeza biashara hiyo ikiwemo utoaji wa elimu ya kutosha kwa jamii 
ili kuwasaidia vijana walioathirika na dawa za kulevya.

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment