Pages

Ads 468x60px

Saturday, June 27, 2015

Mashine ya BVR Yaibiwa Jijini Mwanza, wawili watiwa mbaroni >>



Watu wasiojulikana usiku wa kuamkia jana, waliiba mashine moja inayotumika kwa ajili ya kuandikishia vitambulisho katika daftari la kudumu la wapiga kura (BVR) katika kata ya Kayenze wilayani Magu mkoa wa Mwanza.
 
Akizungumza na mwandishi wetu, kamanda wa polisi wa mkoa wa Mwanza, Charles Mkumbo, amesema mashine hiyo pamoja na nyingine 13, zilienda kuchajiwa katika nyumba ya kulala wageni ya BM Lodgei, lakini asubuhi zilipofuatwa haikuweza kupatikana.
 
Kamanda Mkumbo amesema baada ya kupata taarifa ya kuibiwa mashine hiyo, msako mkali ulifanyika ukiwamo wa kuwahoji wasimamizi wa mashine hizo.

Anasema baada ya kufanyika msako mkali kwa kuweka vizuizi sehemu mbalimbali, walifanikiwa kuikuta ikiwa imetelekezwa njiani ikiwa salama bila kuharibiwa, lakini hakuna mtu aliyeweza kukamatwa.
 
Hata hivyo, kamanda Mkumbo amesema polisi wamefanikiwa kuwashikilia watu wawili wa nyumba hiyo ya kulala wageni kwa mahojiano ili kufahamu mashine hiyo ilivyoweza kutoweka katika mazingira ya kutatanisha.
 
Aidha, ametoa wito kwa waandikishaji kuwa makini pale wanapohifadhi mashine hizo ili zisiweze kuharibiwa ama kuibiwa na watu wengine.

0 comments:

Post a Comment

SHARE