Pages

Ads 468x60px

Monday, June 8, 2015

KAHAMA : Bodaboda 100 wapatiwa mafunzo Kahama>>



WAENDASHA pikipiki 100 wilayani Kahama Mkoa wa  Shinyanga wametakiwa kuacha kuchukulia mambo ya siasa katika mafunzo wanayopewa na wataalamu wa usalama barabarani kwa vile elimu wanayoipata iatawasaidia katika kujikinga na ajali  zisizokuwa za lazima.

Hayo yalisemwa jana na Diwani wa Kata ya Kahama Mjini,  Abas  Omary  alipofunga mafunzo ya siku mbili ya bodaboda yaliyotolewa na wataalamu kutoka Chuo cha Usafirishaji cha Taifa (NIT),   Dare es Salaam.

Alisema   mafunzo hayo  ni kwa manufaa ya waendesha pikipiki na si wanasiasa hivyo  ni bora wanaposikia   kuna mafunzo   kujitokeza kwa wingi hali ambayo itachangia kupata elimu sahihi ya kuhusu usalama barabarani.

“Ninawaomba bodaboda mnaposikia kuna mafunzo ya usalama barabarani ni bora mkajitokeza kwa wingi kwa sababu  katika mafunzo haya lengo  ni kutoa elimu kwa watu zaidi ya 200 lakini kwa sasa ni madereva 100  ndiyo walijitokeza,”alisema.

 Mkufunzi kutoka  NIT, Charles Kisunga,   ni bora mafanikio yakaonekana ikizingatiwa watu hao wamekuwa ndiyo chanzo kikuu cha ajali barabarani.

Alisema mafunzo hayo ni maombi kutokaSerikalini na hadi  sasa yametolewa    Mtwara kwa washiriki   600, Lindi    na Sengerema mkoani Mwanza.

Naye Mbunge wa Jimbo la Kahama, James Lembeli, ambaye ndiye mfadhili mkuu wa mafunzo hayo, alisema  lengo kuu ni kuhakikisha bodaboda wanaepukana na ajali kwa kufuata sheria za usalama barabaarani kwa usahihi.

0 comments:

Post a Comment

SHARE