Pages

Ads 468x60px

Wednesday, June 3, 2015

READ>> Daftari la Wapiga Kura: Wananchi kuandikishwa siku 7 kwa kila kituo kanda ya ziwa (Geita,Simiyu,Mwanza na Shinyanga)......Mwisho tarehe 4 July



Zoezi la Uandikishaji  daftari la kudumu la wapiga Kura linatarajia  kuanza  katika mikoa ya Geita, Simiyu, Mwanza na Shinyanga, zoezi litakaanza rasmi tarehe 2/06/2015 hadi 04/07/2015.
 
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Tume ya Taifa ya uchaguzi imebainisha kuwa zoezi hilo litafanyika kwa kutumia teknolojia ya BVR (Biometric Voters Registration.Vituo vya uandikishaji vitakuwa kwenye vitongoji, mitaa na Vijiji katika kata zote za mikoa hiyo iliyotajwa hapo juu  na vituo vifunguliwa kuanzia saa 2:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni.
 
Watakaohusika ni;
Waliotimiza miaka 18 na watakaotimiza miaka 18 ifikapo mwezi oktoba 2015.
 
Waliojiandikisha  awali kwenye Daftari la kudumu la wapiga ili kuhuisha taarifa zao na kupata kadi mpya.
 
Wananchi wanatakiwa kujiandikisha katika kwenye vituo vilivyoko ndani ya kata zao.
 
Uandikishaji utafanyika kwa muda wa siku saba kwa kila kituo.

0 comments:

Post a Comment

SHARE