Pages

Ads 468x60px

Friday, June 12, 2015

Urais 2015: Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mathias Chikawe Achukua Fomu ya Kugombea Urais!!



Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe akionesha mkoba wenye fomu za kugombea urais katika ukumbi wa mikutano wa NEC mjini Dodoma.
 

**********
 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe jana amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya  kugombea Urais kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi oktoba 2015.
 
Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu Chikawe alisema akiteuliwa na chama chake kugombea nafasi hiyo ataendeleza mapambano zaidi dhidi ya maadui watatu ambao ni ujinga, maradhi na umaskini pamoja na adui mwingine rushwa ambaye  ni adui wa maendeleo.
 
Waziri Chikawe aliongozana na mke wake pamoja na wapambe mbalimbali ambao walikuwa wakimshangilia wakati wa kujibu maswali ya Waandishi wa Habari  katika wa ukumbi wa  Mkutano mkuu wa NEC.

0 comments:

Post a Comment

SHARE