Pages

Ads 468x60px

Friday, June 19, 2015

Ulemavu wa Ngozi Kuazimishwa kila Juni 13



MKURUGENZI Mkuu wa  Shirika  lisilo la Serikali  linalojishughulisha kutetea haki za watu wenye albinism la Under The Same Sun (UTSS) ,Peter Ash, ameupongeza Umoja wa Mataifa kwa kuitangaza June 13 kila mwaka kuwa siku ya watu wenye ulemabu wa ngozi duniani.

Akizungumza hivi karibuni katika ibada maalumu ya kumshukuru Mungu kwa siku ya uelemavu wa ngozi  duniani iliyofanyika  Kanisa la Tanzania Assemblies of God Beacon Mission Christian Centre,  lililoko Mtaa wa Nyamalango Saut Malimbe  jijini Mwanza na kuhudhuriwa na  baadhi  ya wafanyakazi wa UTSS, akiwemo  Mkurugenzi Mtendaji,  Vicky Ntentema, Ash alisema hiyo ni hatua muhimu iliyofikiwa.
 
Alisema amefurahishwa  na  Umoja wa Mataifa kuitangaza siku  hiyo  kwa kuwa anaamini ni hatua nzuri ambayo itasaidia watu wenye ulemavu wa ngozi nchini na duniani kote kupata nafasi ya kujadiliwa haki zao na mataifa mbalimbali.

“Niko hapa kanisani kwa sababu tangu kuibuka kwa mauaji na ukatwaji viungo kwa watu wenye ulemavu wa ngozi Tanzania, nimekuwa nikimuomba Mungu kila siku ili atusaidie na mauaji haya siku moja ibaki historia,watu wanadhani kwamba kwenda kanisani na kutoa sadaka nyingi ndiyo kumcha Mungu , hawajui kuwa  kanisa sio chama cha wakristo bali ni mahali pa watu wanaohitaji huruma, wema na upendo.
 
“Niko hapa  leo kwa ajili ya kuwahudumia walio na uhitaji watu wenye ulemavu wenzangu ambao wanatekwa, wanakatwa viungo vyao wanatemwa mate  na kuuawa, Mwenyezi Mungu anataka mambo matatu  tu kutoka kwetu  wanadamu  ambayo ameyataja katika kitabu kitakatifu cha biblia Mika aya ya 8 nayo ni kutenda haki,kupenda kuwa na rehema na kutembea kwa unyenyekevu mbele zake,”alisema Ash.

Alisema  kila mkristo, inampasa atafute haki kwa ajili ya watu wenye albinism maana   siku ya mwisho wa maisha ukifika Mungu ndiye atakuwa muendesha mashtaka na jaji ambapo wale ambao hawakutenda haki kwa kuwauwa  na kuwafanyia ukatili watu wenye albinism watashitakiwa maana kutenda haki ni agizo la mwenyezi Mungu.
 
Naye Mchungaji wa kanisa hilo, Valentine Mbuke  alisema binadamu wote wameumbwa na Mungu hivyo ni wajibu wa kila mmoja kutenda haki hakuna aliye na haki ya kuwanyima watu wenye albinism au binadamu mwenzie haki ya kuishi au kuthaminiwa.

0 comments:

Post a Comment

SHARE