Mbunge
wa Tarime Vijijini, John Heche amefunguka na kusema kwa kuwa Rais
Magufuli kupitia ripoti ya pili ya mchanga amesema kampuni ya ACACIA ni
feki na haipo basi yeye anawaambia wananchi wa jimbo lake wajiandae
kuingia mgodini kuchukua kila kitu.
Showing posts with label Politics. Show all posts
Showing posts with label Politics. Show all posts
Wednesday, June 14, 2017
Mbowe Apata Pigo Tena.... Serikali 'Yaharibu' Mitambo Shambani Kwake
Mbunge
wa Hai na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amezidi kukumbwa na
matukio mbalimbali baada ya jana Baraza la Taifa la Uhifadhi na
Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kung’oa mitambo ya umwagiliaji iliyopo
katika shamba lake na kumtoza faini kwa kuendesha kilimo eneo
lisiloruhusiwa.
Msaidizi Wa Mbowe ( Profesa Abdallah Safari ) Amfananisha Rais Magufuli Na Mashujaa Wa Afrika
Kada
wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambaye pia ni Makamu
Mwenyekiti wa Chama hicho, Profesa Abdallah Safari amemfagilia Rais
Magufuli kwa kupigania rasimali za taifa ikiwemo madini yaliyokuwa
yakiwanufaisha Wawekezaji.
LOWASSA: Avunja ukimya na kuonyesha uzalendo wake kwa kumpongeza Rais Magufuli..soma hapa
“Nimpongeze sana Mhe Rais John Pombe
Magufuli kwa uamuzi na hatua ambazo amechukua kuhusu jambo hili, na hasa
pale anapowashirikisha wananchi, ni jambo muhimu sana.
UNICEF YASAIDIA VITANDA VYA WAGONJWA WA KIPINDUPINDU ZANZIBAR!
Waziri
wa Afya, Mahmoud Thabit Kombo akipokea msaada wa vitanda vya wagonjwa
wa kipindupindu kwa Afisa Mkaguzi Mkuu wa Shirika la kuhudumia watoto
Duniani (UNICEF) Bi. Francesca Morandini katika kambi ya kipindupindu
Chumbuni.
Tuesday, June 13, 2017
Spika Job Ndugai Atoa ONYO Kwa Halima Mdee na Ester Bulaya......Atishia Kuwapa Adhabu Kali Zaidi
Spika
wa Bunge Mhe. Job Ndugai leo bungeni amewapa onyo wabunge Halima Mdee
pamoja na Easter Bulaya akisema kuwa wanapaswa kutambua kuwa Bunge bado
linauwezo wa kuwaita na kuwahoji na kuwapa adhabu kali zaidi ya hiyo
walionayo sasa.
Rais Magufuli Akutana na Wakuu Wote wa Mikoa Nchini na Kutoa Maagizi Mazito
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli
amewaagiza Wakuu wa Mikoa kusimamia kwa ukaribu utekelezaji wa mpango wa
ujenzi wa viwanda katika maeneo yao ili kuwawezesha wananchi kuongeza
thamani ya mazao yao na kuzalisha ajira.
Profesa Kitila Mkumbo Awapa Makavu Wapinzani Wanaopinga Ripoti za Rais Magufuli
Katibu
Mkuu wa wizara ya maji na umwagiliaji, Profesa Kitila Mkumbo
amewakejeli watu wanaopinga ripoti mbili za mchanga zilizowasilishwa na
tume mbili tofauti za wasomi kwa Rais John Magufuli.
Serikali yatoa kibali cha kuajiri watumishi 15000 kuziba nafasi za watumishi waliobainika kuwa na vyeti feki.
Waziri
wa nchi,Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora Mh.Angela Kairuki
amesema tayari serikali imeshatoa kibali cha ajira 15000 kwa ajili ya
kujaza nafasi zilizoachwa wazi na watumishi waliobainika kuwa na vyeti
feki katika zoezi lililofanyika nchi nzima la kuwabaini na muda si mrefu
nafasi hizo zitajazwa.
Spika Jobu Ndugai Atoa ONYO Kwa Wabunge wa Upinzani Wanaotaka Marais Wastaafu Washitakiwe
Spika
wa Bunge, Job Ndugai amewakumbusha wabunge wa upinzani wanaotaka marais
wastaafu washtakiwe kuhusu sakata la mchanga wa madini, wakumbuke wanao
mawaziri wakuu wastaafu wawili ambao watahusika pia.
Waziri Mkuu Majaliwa awavalisha vyeo Maafisa wa Magereza, ahimiza haki na usawa
Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa amewataka
maaafisa na makamanda wa Jeshi la Magereza nchini waendelee kusimamia
haki na usawa wanapotimiza wajibu wao.
Maoni ya Tundu Lissu baada ya Rais Magufuli kupokea ripoti ya pili ya kamati maalum ya uchunguzi wa madini
For the Record: What Goes Around Comes Around!!!
Leo wapinzani wa Serikali ya Magufuli tumesemwa sana na kutishiwa kushughulikiwa bungeni na nje ya Bunge.
Walichokisema Dr Kafumu, Ngeleja na Andrew Chenge Baada ya Kutakiwa Kuhojiwa Na Vyombo vya Dola
Vigogo
waliotajwa katika ripoti ya pili ya kuchunguza makontena yenye mchanga
wa madini (makinikia) kuisababishia Serikali hasara ya matrilioni ya
fedha kupitia sekta ya madini, walipokuwa wakihudumu katika nyadhifa zao
serikalini wamevunja ukimya.
Prof. Muhongo, Andrew Chenge na Wahusika Wengine Wazuiwa kutoka nje ya Mipaka ya Tanzania
Serikali
imeagiza, Mawaziri, Wanasheria Wakuu wa Serikali na Manaibu wao,
Wakurugenzi wa idara za mikataba, na Makamishna wa madini, wanasheria wa
Wizara ya Nishati na Madini na watumishi wengine wa Serikali na watu
wote waliohusika katika kuingia mikataba ya uchimbaji madini, utoaji wa
leseni za uchimbaji wa madini na kuongeza muda wa leseni, watumishi na
wamiliki wa makampuni ya madini kuto toka nje ya mipaka ya Tanzania.
Monday, June 12, 2017
ACACIA wapinga vikali matokeo ya kamati ya pili ya Rais
Mwitikio wa Acacia kwenye matokeo ya kamati ya pili ya Rais
Acacia imeona matokeo ya kushtua ya kamati ya pili ya Rais iliyowasilishwa kwa Rais wa Tanzania Mh. Dk John P. Magufuli leo asubuhi ambayo imeangalia nyanja za historia za kiuchumi na kisheria ya mauzo ya nje ya makanikia ya madini.
Acacia imeona matokeo ya kushtua ya kamati ya pili ya Rais iliyowasilishwa kwa Rais wa Tanzania Mh. Dk John P. Magufuli leo asubuhi ambayo imeangalia nyanja za historia za kiuchumi na kisheria ya mauzo ya nje ya makanikia ya madini.
FULL RIPOTI: Hii Ndo Taarifa Yote Ya Kamati ya Pili ya Kuchunguza Madini Katika Mchanga Iliyowasilishwa Kwa Rais Leo
Leo June 12, 2017 Rais Magufuli amepokea Ripoti ya piti ya kamati aliyounda kuchunguza madini katika mchanga.
Spika Job Ndugai kuunda timu ya kuchunguza suala la madini ya Almasi
Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema ataunda timu yake itakayofuatilia suala la madini ya almasi.
Ndugai
ameyasema hayo leo baada ya kamati ya pili kutoa ripoti yake kuhusu
mchanga wa madini katika makontena 277 yanayoshikiliwa.
Wapinzani Walivyosimama Bungeni na Kuanza Kuimba Wana Imani na Mkapa, Kikwete
Bunge
limezizima kwa makofi baada ya hotuba ya mpango wa bajeti ya kambi
rasmi ya upinzani.Wabunge wa upinzani ndiyo wengi waliobaki ukumbini
baada ya wengi kwenda kufuatilia ripoti ya kamati ya pili ya Rais John
Magufuli kuhusu usafirishaji wa makinikia.
Profesa Muhongo Kitanzini Tena.....Ni Baada ya Rais Magufuli Kuviagiza Vyombo vya Dola Vimuhoji Kwa Kusaini Mikataba Mibovu ya Madini

Rais
wa Jamhuri ya Muungano, Dkt Magufuli ameagiza viongozi wa Wizara ya
Nishati na Madini, Manaibu wake, Wanasheria Wakuu wa Serikali, Makatibu
Wakuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Maafisa wa TRA, na watumishi
wengine waliohusika katika upotevu wa matrilioni ya fedha kupitia sekta
ya madini wahojiwe.
Subscribe to:
Posts (Atom)

















