KIWANGO cha kiungo wa AFC Leopards, Allan Kateregga kwenye michuano ya Super Cup, kimewavuta Simba na sasa wanataka kunasa saini ya nyota huyo wa Kenya.
Kiungo huyo aliingia kipindi cha pili katika mchezo wao wa Super Cup dhidi ya Singida United na kutoa pasi ya bao kwa Vincent Oburu aliyeisawazishia timu yake na kutinga nusu fainali kwa mikwaju ya matuta 5-4, akiwamo kwenye orodha ya wapigaji.

